Serikali itaendelea kusimamia utoaji wa matibabu kwa Wazee bila malipo, upatikanaji wa dawa Hospitalini na uwepo wa dirisha maalum kwa ajili ya Wazee ili kuwaenzi na kuwaondolea usumbufu.
Kauli hiyo imetolewa leo na Mkuu wa wilaya ya Singida Mjini Mhandisi Paskasi Muragili kwaniaba ya Mkuu wa mkoa wa Singida wakati wa Maadhimisho ya Siku ya wazee Duniani yaliyofanyika mjini Singida.